Chuo Kishiriki cha Elimu cha Mkwawa kimesaini Mkataba wa Makubaliano (MoU) na Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) kwa ajili ya utoaji wa huduma za matibabu ya haraka kwa wafanyakazi wa Chuo. Hafla ya utiaji saini wa mkataba huo imefanyika tarehe 13 Januari 2025.
Mkataba huo umesainiwa na Rasi wa Chuo, Profesa Method S. Semiono, na Profesa Abel Makubi, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa.
