Sekta ya kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi—lakini mabadiliko ya tabianchi yameendelea kutishia uzalishaji na maisha ya wakulima wetu. 🌍
Kupitia ushirikiano wa MUCE, TARI, Enviroenergies na WiN-TZ, watafiti wamezindua rasmi mradi wa ECSA-SATZ, unaolenga kuwawezesha wakulima wadogowadogo wa Manyoni (Singida) na Bahi (Dodoma) kukabiliana na athari za tabianchi kupitia kilimo himilivu.