Leo, tarehe 28 Agosti 2025, MUCE ilipata heshima ya kutembelewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Kheri James, aliyefika Chuoni kuangalia maendeleo ya miradi ya ujenzi wa miundombinu mipya inayotekelezwa na Chuo. Katika ziara hiyo, kabla ya kutembelea miradi ya ujenzi, Mkuu wa Mkoa alipewa taarifa ya safari ya Chuo, mafanikio yake, na mchango wake katika kukuza elimu ya juu nchini.