Skip to main content

KITUO CHA MFANO CHA MALEZI YA WATOTO MUCE

Date: 22 Dec 2025
Usajili kwa mwaka 2026 umefunguliwa. Kituo kipo ndani ya Chuo Kishiriki cha Elimu Mkwawa na Kinafanya shughuli zake kwa mujibu wa sheria na taratibu za Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Wazee na Watoto. BOFYA HAPA Kupakua fomu ya kujiunga

Ujumbe karibishi kutoka kwa mkuu wa chuo

Ninafuraha kubwa kukukaribisha Chuo Kishiriki cha Elimu Mkwawa (MUCE), chuo kishiriki cha Chuo kikuu cha Dar es Salaam kilichopo katika mji wa kihistoria Iringa, Tanzania.

Hapa MUCE, tunajivunia kutoa digrii za awali na za uzamili zinazowapa wahitimu wetu si tu maarifa ya kitaaluma kinadharia, bali pia ujuzi wa kivitendo unaohitajika ili kufanikiwa kwenye tasnia ya elimu inayobadilika kila uchao. Wana kitivo mahiri na makini wanajitolea kudumisha viwango vya juu kabisa vya ufundishaji na utafiti, kuhakikisha kila mwanafunzi anapata mazingira rafiki na jumuishi ya ujifunzaji.

Kama Mkuu wa Chuo, ninakualika ujionee utajiri wa fursa na rasilimali zinazopatikana MUCE. Ikiwa wewe ni mwanafunzi tarajali, mzazi au taasisi mshirika, ninakuomba ujionee jinsi uwajibikaji wetu katika ujenzi wa elimu bora, uvumbuzi na huduma unavyoweza kukusaidia kufikia matarajio yako.

Asante kwa kutembelea tovuti yetu. Tunatazamia kukukaribisha wewe binafsi na kukuongoza kuelekea kwenye mustakabali uliojengwa na mafanikio ya kitaaluma na wenye matokeo yenye tija.

Prof. Method Samwel Semiono
Mkuu wa Chuo, Chuo Kishiriki cha Elimu Mkwawa (MUCE)

Digrii za Awali

Digrii za Uzamili

403
Wafanyakazi
6272
Wanafunzi
16548
Idadi ya wahitimu
1
Ngazi na utambuzi