MUCE imesheheni miti ya asili na ya kupandwa, nyasi na maua. Kampasi hii ina eneo la Ekari 633.31, ambapo eneo lililoendelezwa ni Ekari 114.71, sawa na 18.11%, na eneo ambalo bado halijaendelezwa ni Ekari 518.60, sawa na 81.89% ya eneo lote. Matumizi ya ardhi iliyopo yamegawanywa katika maeneo mbalimbali. Ambayo ni eleo la utawala, eneo la mabweni ya wanafunzi, eneo la kituo cha afya, eneo la burudani, eneo la biashara na eneo la miliki. Eneo la Taalama ni 5.01% ya ardhi yote. Eneo hili linajumuisha Kumbi za Mihadhara, Vyumba vya Mihadhara, Vyumba vya Semina, Maabara za Sayansi, Maabara za Kompyuta, Kituo cha Rasilimali za Midia za Elimu na Maktaba.






