📍 16 Mei 2025 | Chuo Kishiriki cha Elimu Mkwawa (MUCE)
Leo tarehe 16 Mei 2025, Chuo Kishiriki cha Elimu Mkwawa (MUCE) kimepokea kwa heshima ujio wa Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Iringa. Ujumbe huo umeongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa, Comrade Daud Yassin, ukiwa na lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu inayotekelezwa kupitia Mradi wa Higher Education for Economic Transformation (HEET).